Welcome to my blog!

Meet the Author

Ut eleifend tortor aliquet, fringilla nunc non, consectetur magna. Suspendisse potenti.

Looking for something?

Subscribe to this blog!

Receive the latest posts by email. Just enter your email below if you want to subscribe!

Tuesday 15 July 2014

Moto uliozuka leo umeteketeza Nyumba nzima Mwananyamala, na hii ni taarifa ya Jeshi la Polisi.



Moto ambao Madhara yake yanayonekana kwa sasa ni pamoja na kuteketeza nyumba ya vyumba 12 pamoja na mali zote zilizokuwemo ndani ya vyumba,pamoja na vyumba 4 vya biashara vilivyopo nje ya barabara.
Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Kinondon kamishna msaidizi wa polisi Camellius Wambura amethibitisha kutokea kwa moto huo na kusema Moto huo umetokea leo majira ya saa 5 na nusu mtaa wa Malanga eneo la Mwanayamala.
Nyumba iliyotoketea kwa moto imetajwa mmiliki wake kuwa ni mzee abdalah, ambaye alikuwa akimiliki nyumba mbili zilizopakana katika eneo hilo zote zikiwa zina vyumba 12,chanzo cha moto huo kinasemekana ni hitilafu ya umeme.
Wananchi wa eneo hilo wamelalamikia hali ya Kikosi cha Zimamoto na Uokoaji kuchelewa kufika eneo la tukio.
Baadhi ya picha katika tukio hilo 



source:millardayo.com