Wanajeshi 480 wa Nigeria
wametorokea maisha yao nchi jirani ya Cameroon kufuatia makabiliano
makali dhidi ya wapiganaji wa kundi la kiislamu la Boko Haram.
Msemaji wa jeshi la Cameroon Luteini Kanali
Didier Badjek amethibitisha kisa hicho na kusema kuwa wamepokonywa
silaha na sasa wamewekwa katika shule .
Mapigano hayo yanawadia saa chache tu baada ya
wapiganaji hao wa Boko Haram kutoa kanda ya video ambayo walitangaza
kuundwa kwa himaya ya Kiislamu kaskazini Mashariki mwa Nigeria.
Haijabainishwa iwapo Bwana Shekau ameahidi kutii
Muungano wa wapiganaji wa kundi la kiislamu la Islamic State
inayotawala sehemu kubwa ya Kaskazini mwa Iraq na Syria.
Msemaji wa Jeshi la Nigeria Chris Olukolade alipinga tangazo hilo akisema kuwa ''hakuna hata nchi moja ya taifa hilo iliyotwaliwa na kuwa Nigeria ni moja. ''
Maelfu ya watu wameuwawa kaskazini mashariki mwa Nigeria tangu 2009, wakati Boko Haram ilipoanza uasi wake. Gwoza, iliyokuwa na wakazi 265,000 katika sensa iliyopita, ndiyo mji mkubwa zaidi ulio chini ya utawala wa Boko Haram.
Imepeperusha bendera zake juu ya Kasri ya Emir wa Gwoza, kiongozi wa kiasili wa mji huo, wakazi wanasema.
Kiongozi wa Boko Haram Abubakar Shekau
alizungumza kwenye kanda ya video iliyotolewa ili kupongeza wapiganaji
wake kwa kuchukua udhibiti wa mji wa Gwoza mapema mwezi huu.
Msemaji wa Jeshi la Nigeria Chris Olukolade alipinga tangazo hilo akisema kuwa ''hakuna hata nchi moja ya taifa hilo iliyotwaliwa na kuwa Nigeria ni moja. ''
Kiongozi wa Boko Haram Shekao ametangaza himya ya KIislamu Kaskazini mashariki mwa Nigeria
Imepeperusha bendera zake juu ya Kasri ya Emir wa Gwoza, kiongozi wa kiasili wa mji huo, wakazi wanasema.
